Zubeidah Kananu
Zubeidah alijiunga na kampuni ya Standard Januari Mwaka 2007. Alipitia mafunzo kwa muda wa miezi mitatu kisha akafanya kazi kwa kandarasi kwa muda wa mwaka mmoja.
Mwaka 2009 aliajiriwa kama mfanyakazi wa kudumu na kuwa ripota wa KTN. Alipandishwa daraja miezi michache baadaye na kuwa ripota mkuu. Mwaka 2012 alipandishwa daraja tena na kuwa mhariri wa masuala ya kisiasa katika meza ya KTN LEO. Yeye pia ni mtayarishi wa taarifa za KTN LEO mbali na kuwa msomaji habari wa taarifa kwa lugha ya Kiswahili.